Application Form for Academic Year 2023/2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tanzanian Training Centre for International Health, (TTCIH) anawatangazia umma nafasi za kujiunga na chuo kwa mwaka wa masomo 2023/2024. TTCIH ni taasisi ya mafunzo ya Afya Ifakara iliyosajiliwa na NACTVET kwa namba HAS/003, Chuo kipo Ifakara mjini, Mkoani Morogoro. Chuo kina mazingira tulivu na mazuri kwa kujifunza ikiwa pamoja wakufunzi wabobezi katika masomo yote, Hospitali ya kujifunzia, maktaba bora na masomo kwa njia ya kielektroniki yaani eLearning.

Chuo Kinatoa Kozi Zifuatazo

  1. Stashahada ya Utabibu (Diploma in Clinical Medicine) – Miaka Mitatu
  2. Stashahada ya Utabibu ya Mwaka Mmoja (Yaani upgrading from Clinical Assistant to Clinical Officer).
  3. Stashahada ya Ufamasia (Diploma in Pharmaceutical Sciences) – Miaka mitatu
  4. Stashahada ya Optometria (Diploma in Optometry) – Miaka mitatu
  5. Stashahada ya Health Information Sciences – Miaka mitatu
  6. Higher Diploma in Clinical Medicine – Miaka miwili

Sifa za Mwombaji kwa Kozi ya Stashahada ya Utabibu ya Miaka Mitatu awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Chemistry na Physics

Sifa za Mwombaji wa Stashahada ya Utabibu Mwaka Mmoja (Yaani Upgrading From Clinical Assistant to Clinical Officer ) awe :

  • Amehitimu Astashahada ya Utabibu (Technician Certificate in Clinical Medicine).

Sifa za Mwombaji kwa kozi ya stashahada  ya Ufamasia (miaka mitatu) awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufaulu wa angalau D ya Biology na Chemistry

Sifa za Mwombaji kwa kozi ya stashahada  ya Optometria (Miaka mitatu) awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Chemistry, Basic Mathematics, English  na Physics/Engineering Sciences

Sifa za Mwombaji kwa kozi ya stashahada  ya Health Information Sciences  (Miaka mitatu) awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Basic Mathematics na English Language

Sifa za Mwombaji kwa kozi ya stashahada  ya Higher Diploma in Clinical Medicine (Miaka miwili) awe :

  • Amehitimu Stashahada ya Utabibu (Diploma in Clinical Medicine) kwa ufaulu angalau kwanzia GPA ya 2.7 pia awe amefanya kazi ya Utabibu sio chini ya MIAKA MIWILI.

Jinsi ya Kujaza Fomu za Maombi

Maombi yote ya kujiunga na Chuo yanatumwa kupitia tovuti ya NACTVET  kwenye kiunganishi (QUICK LINK ) kilichoandikwa MAOMBI YA UDAHILI VYUO VYA AFYA 2023, Kwa msaada wa kujaza FOMU MOJA KWA MOJA CHUONI, tafadhali jaza taarifa zako kwenye hii fomu hapa chini  kisha bofya “SEND” dawati la usajili litakupigia simu  muda wowote kukusaidia kujaza fomu kikamilifu au piga simu namba zifuatazo (+255) 0718552164, 0718365374, 0710527003 & 0758943044

KARIBU TTCIH IFAKARA KWA MAFUNZO YENYE KUJENGEA WAHITIMU UWEZO KUTOA TIBA KWA KUTUMIA TAFITI YAANI  EVIDENCE BASED MEDICINE

 

Our Clients Reviews & Testimonials

TouchAnd CleanCompany
TouchAnd CleanCompany
5. August, 2022.
Nice
Thomas Mathayo
Thomas Mathayo
2. August, 2022.
Nice
allypeter tv
allypeter tv
29. May, 2022.
It’s a good college for clinical officers
Diman Shilla
Diman Shilla
7. April, 2022.
Awesome

Share: