Application Form for Academic Year 2023/2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tanzanian Training Centre for International Health, (TTCIH) anawatangazia umma nafasi za kujiunga na chuo kwa mwaka wa masomo 2023/2024. TTCIH ni Taasisi ya mafunzo ya Afya Ifakara iliyosajiliwa na NACTVET kwa namba HAS/003, Chuo kipo Ifakara mjini, Mkoani Morogoro. Chuo kina mazingira tulivu na mazuri kwa kujifunza ikiwa pamoja wakufunzi wabobezi katika masomo yote, Hospitali ya kujifunzia, maktaba bora na masomo kwa njia ya kielektroniki yaani eLearning

Chuo Kinatoa Kozi Zifuatazo

  • Stashahada ya Utabibu (Diploma in Clinical Medicine) – Miaka Mitatu
  • Stashahada ya Utabibu ya Mwaka Mmoja (Yaani upgrading from Clinical Assistant to Clinical Officer).
  • Stashahada ya Ufamasia (Diploma in Pharmaceutical Sciences) – Miaka mitatu
  • Stashahada ya Optometria (Diploma in Optometry) – Miaka mitatu
  • Stashahada ya Health Information Science – Miaka mitatu

Sifa za Mwombaji kwa Kozi ya Stashahada ya Utabibu ya Miaka Mitatu awe

  • Awe amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Chemistry na Physics

Sifa za Mwombaji wa Stashahada ya Utabibu Mwaka Mmoja (Yaani Upgrading From Clinical Assistant to Clinical Officer )

  • Awe  amehitimu Astashahada ya Utabibu (Technician Certificate in Clinical Medicine).

Sifa za muombaji kwa kozi ya stashahada  ya Ufamasia (miaka mitatu) awe na:

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufaulu wa angalau D ya Biology na Chemistry

Sifa za muombaji kwa kozi ya stashahada  ya Optometria (Miaka mitatu) awe na:

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Chemistry, Basic Mathematics, English  na Physics/Engineering Sciences

Sifa za muombaji kwa kozi ya stashahada  ya Health Information Sciences  (Miaka mitatu) awe na:

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Basic Mathematics na English Language

Jinsi ya Kujaza Fomu za Maombi

  • Maombi yote ya kujiunga na Chuo yanatumwa kupitia tovuti ya NACTVET  kwenye kiunganishi (QUICK LINK ) kilichoandikwa MAOMBI YA UDAHILI VYUO VYA AFYA 2023, Kwa msaada wa kujaza FOMU MOJA KWA MOJA CHUONI, tafadhali jaza taarifa zako kwenye hii fomu hapa chini  kisha bofya “SEND” dawati la usajili litakupigia simu  muda wowote kukusaidia kujaza fomu kikamilifu au piga simu namba zifuatazo (+255) 0758943044, 0787629707, 0710527003 & 0718365374.

KARIBU TTCIH IFAKARA KWA MAFUNZO YENYE KUJENGEA WAHITIMU UWEZO KUTOA TIBA KWA KUTUMIA TAFITI YAANI  EVIDENCE BASED MEDICINE

 

Our Clients Reviews & Testimonials

[trustindex no-registration=google]

Share:

    This will close in 10 seconds

    error: CONTENT IS PROTECTED !!