Taasisi ya Mafunzo ya Afya TTCIH – IFakara inapenda kutoa taarifa kwa umma kwamba matokeo ya uchaguzi awamu ya kwanza kwa waombaji wa programu ya Utabibu (Yaani Diploma in Clinical Medicine) mkupuo wa Septemba 2022/2023 yametoka rasmi leo tarehe 15 Agosti, 2022. Waombaji wote waliochaguliwa wanaweza kupakua maelekezo ya kujiunga na Chuo (Joining Instructions) kwenye kiunganishi hapa chini kwa ajili ya kupata taarifa zaidi.